Thursday, July 11, 2013

TANZANIA NI YA 12 KWA UFISADI,KENYA YAONGOZA SOMA LIPOTI HII.

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Transparency International, Tanzania imeshika nafasi ya kumi na mbili kwa ufisadi ikiwa ni miongoni mwa nchi 107 ambako utafiti huo ulifanywa ukihusisha wananchi 1001 wa Tanzania.

Ripoti hiyo ilibaini kwamba Watanzania karibia sita kati ya 10 waliohojiwa walisema wamewahi kutoa hongo maishani mwao ili waweze kupata huduma moja hadi nane kati ya zilizochunguzwa.

Kulingana na utafiti huo, wananchi 87% walisema maofisa wa polisi ndio wanaongoza kwa ruswa wakifuatiwa na mahakama (86%) hospitalini (79%), wafanyakazi wa serikali (75%) sekta ya elimu (74%) na vyama vya siasa (68%)

Watanzania 23% walisema taasisi za kidini zinajihusisha na ruswa wakati Jeshi (38%) na vyombo vya habari (41%).

Asilimia 3 ya Wakenya na Watanzania waliohojiwa walisema rushwa imepungua tofauti na asilimia 56 ya Warwanda huku asilimia 1 ya Waganda na Warundi wakidai vivyo hivyo.

Nchi fisadi zaidi duniani ni Sierra Leone ambako asilimia 84 ya watu waliohojiwa walikubali kwamba wametoa hongo. Sierra Leone inafuatwa na Liberia (asilimia 75) na Yemen (asilimia 74).

Nchi ambazo zilipatikana kuwa na ufisadi finyu ni Finland, Japan, Australia, Denmark, Uhispania, Canada, Ureno, Uruguay, Norway, New Zealand, Korea Kusini na Malaysia ambako watu zaidi ya 95 kati ya 100 waliohojiwa walisema hawajaona ufisadi wowote nchini mwao.

Katika eneo la Afrika Mashariki, Kenya ndiyo nchi fisadi zaidi ikifuatwa na Uganda (asilimia 61) na Tanzania (asilimia 56). Kulingana na utafiti huo ambao watu 114,000 walihojiwa, Rwanda ilipatikana kuwa na ufisadi mdogo zaidi katika eneo la Afrika Mashariki. Raia 13 pekee kati ya 100 wa nchi hiyo walikubali mwamba wametoa hongo. Ufisadi ulipatikana kukithiri zaidi barani Afrika. Baadhi ya nchi fisadi zaidi Afrika ni Zimbabwe, Msumbiji, Libya na Cameroon (zote zikiwa na asilimia 62) na Nigeria (asilimia 44).

Njia iliyotumia ni kwa kupata maoni kwa njia ya maswali ambapo wananchi zaidi ya 1000 kwa kila nchi 107 walihojiwa na kujibu maswali uso kwa uso na kwa njia ya elecroniki kati ya Sept 2012 mpaka March 2013.

Kwa nchi za afrika ya mashariki, wananchi walihojiwa kwa njia ya uso kwa uso na makampuni ya TI kenya, TI Rwanda na Infinite insight katika maeneo ya mjini na vijijini.

Ripoti hii imechapishwa na
SSUU - Global Corruption Barometer 2013 by Transparency International


No comments:

Post a Comment