Friday, August 2, 2013

TANZANIA KUKUTWA,KUVUTA BANGI NI KOSA BUNGE URUGUAY LAIDHINISHA BANGI KAMA ZAO LA BIASHARA.

Hama kweli sasa sijui ndo Maendeleo yanazidi katika Dunia hii au ndo haki inafuatwa wakati baadhi ya Nchi zao la Bangi linapigwa marufuku na uvutaji wake pia ni kosa lakini hali ni tofauti katika nchi ya Uruguay baada ya hivi majuzi Bunge la nchi hiyo kupitisha

 muswada wa sheria wa kuidhinisha matumizi ya bangi.Kutokana na kura zilizopigwa bungeni,kati ya wabunge 94,wabunge 50 wamepiga kura ya kukubali matumizi ya bangi.
Sheria hiyo inaonyesha kwamba serikali pekee ndiyo itakayosimamia na kufungua na kumiliki maduka hayo kwasababu wafanya biashara binafsi wamekua wakiuza 'kijiti'hicho kwa bei ya juu na kupata faida kubwa na kuleta usumbufu mkubwa kwa wananchi wake.
Pia sheria hiyo inasema kwamba wageni hawataruhusiwa kununua bangi hiyo na kila mteja anatakiwa kua na kitambulisho kinachoonyesha uraia wake na umri wake,na pia wateja wote watakua wakiolozeshwa kwenye daftari maaulumu kwa ajiri ya kutoa bonus kwa mteja aliyenunua mara nyingi!!!

Kitendo hicho cha kupitisha mswada huo kimeufanya  Umoja wa Mataifa washutumu hatua hiyo.

No comments:

Post a Comment