Thursday, February 6, 2014

TEKNOLOJIA MLEMAVU WA MKONO AWEKEA MKONA WA KIELECTRONIKI .

Mlemavu mmoja kutoka Denmark Dennis Aabo amekuwa binadamu wa kwanza kupewa mkono wa kieletroniki wenye hisia kama ule wa binadamu.

Katika tukio linalopigiwa upatu kuimarisha hali ya walemavu katika siku za usoni, madaktari huko Italia wameuunganisha mkono huo wa kielektroniki na neva za mabaki ya mkono wa Dennis uliokatwa baada ya ajali mbaya ya fataki na hivyo kumwezesha kuhisi kupitia kwa vidole vya mkono huo wa kielektroniki .

 

Silvestro Micera aliyeongoza upasuaji huo alifurahishwa mno na uwezo wa mgonjwa wake kuutumia mkono huo bandia .

'' tumeshangazwa sana na urahisi wa mgonjwa wetu kuwasiliana mara moja na mkono huu bandia wa kielektroniki kuekelea majukumu ya kushika na kuhisi vitu tofauti .
Hata ikiwa upasuaji huu utakuwa wa muda tu, ninahakika Denis ameotambua mwenyewe kuwa utakuwa wenye manufaa makubwa kwake katika siku za usoni''

Mkono bandia wa kielectroniki

Dennis hakuficha furaha yake alisema mkono huo umebadilisha kabisa hali yake.
''hisia zangu za mkono zimeimarika maradufu maanake ninawezajua ugumu na mfumo wa kitu chochote ni kama mkono wa kawaida'' 

 Mfumo wa mkono wa Kielektroniki

Habari hii imenukuliwa kama ilivyo kutoka BBC.


No comments:

Post a Comment